Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Syria yaitenga Marekani, makubaliano ya tabia nchi ya Paris.

  • November 8, 2017
Syria yaitenga Marekani katika, makubaliano ya tabia nchi ya Paris

Marekani inakaribia kutengwa kutokana na msimamo wake kuhusu makubaliano ya tabia nchi baada ya Syria kusema kuwa iko tayari kuunga mkono makubaliano hayo.

Makubaliano hayo ya Paris yanaunganisha mataifa duniani katika kukabiliana na hali ya tabia nchi.

Syria na Nicaragua yalikuwa mataifa ya pekee nje ya makubaliano hayo wakati yalipotiwa saini 2015.

Nicaragua ilitia saini yake mnamo mwezi Oktoba.

Mnamo mwezi Juni Marekani ilisema kuwa itajiondoa , lakini sheria za mkataba huo zinasema kuwa hatua hiyo haiwezi kufanyika hadi 2020.

Wakati huohuo maafisa wa Ufaransa wamesema kuwa rais Donald Trump hakualikwa katika mkutano wa wa Disemba kuhusu hali ya tabia nchi utakaofanyika mjini Paris.

Zaidi ya mataifa 100 yamealikwa katika mkutano huo ambao unalenga kujenga miungano ya kifedha na kibishara ili kuimarisha mkataba huo kulingana na msaidizi wa rais Emmanuel Macron.

Akitangaza uamuzi huo wa Marekani mnmao mwezi Juni, rais Trump alisema kuwa ni wajibu wake kuilinda Marekani na kwamba atakubaliana na mkataba mpya ambao hautaathiri biashara za Marekani.

Alidai kwamba mkataba huo utagharimu kazi milioni 6.5 za Wamarekani na dola trilioni 3 za uchumi wake, huku washindani wake wakuu kama vile China na India wakipendelewa na makubaliano hayo.

Taarifa ya Marekani iliotolewa mwezi Oktoba baada ya Nicaragua kutia saini makubaliano hayo ilisema kuwa Marekani itajiondoa hadi pale mkataba huo utakapoipendelea.

Msemaji wa Ikulu ya Whitehouse Kelly Love amesema kuwa hakuna mabadiliko yoyote kuhusu msimamo huo

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Donald Trump amuonya Kim Jong-Un moja kwa moja.
Picha za tembo waliochomwa moto yashinda tuzo

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise