Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Halmashauri ya Manispaa ya TABORA imeshauriwa kuweka utaratibu…

  • January 30, 2018

Halmashauri ya Manispaa ya TABORA imeshauriwa kuweka utaratibu mzuri wa uzoaji wa taka katika dampo la KACHOMA ili kukabiliana na mrundikano wa uchafu unaokuwepo mara kwa mara.

Baadhi ya wafanyabiashara katika soko la KACHOMA,SAIDI JUMA na SHABANI MASHAKA wamesema mrundikano wa uchafu katika eneo hilo unatokana na kutozolewa taka kwa wakati na idadi ndogo ya makontena.

Naye mfanyabiashara mwingine katika soko hilo,HALFAN KABATA amesema  dampo la KACHOMA linasababisha wadudu wasambae maeneo ya biashara zao.

Kwa upande wake,Katibu wa soko hilo,ALI KAFWIMBI amesema tatizo kubwa linalochangia mrundikano wa taka katika dampo hilo ni kuwepo kwa gari moja pekee la kuzolea taka.

Amewataka wananchi kuacha tabia ya kumwaga takataka katika eneo hilo na kwamba kila mmoja awe mlinzi wa mwenzake kwa sababu viongozi wana majukumu mengi hivyo ni vigumu kuwasimamia kutomwaga uchafu katika eneo hilo.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Halmashauri ya manispaa ya TABORA imeshindwa kukusanya asilimia 50 ya mapato ya ndani katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2017-2018.
Odinga ala kiapo uwanja wa Uhuru Park

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise