Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Jamii yatakiwa kuwaelimisha wanawake ambao bado hawajaelimika kuhusu…

  • March 7, 2018

Jamii mkoani TABORA imetakiwa kuwaelimisha wanawake ambao bado hawajaelimika kuhusu haki zao. Mwalimu wa shule ya msingi ISIKE mjini TABORA,VAILETH KIRIGITO amesema katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani inayofanyika Machi Nane kila mwaka,wanawake walioelimika wanatakiwa kuwaelimisha wenzao ambao hawajazitambua haki zao za msingi. 

Naye Mwalimu LETICIA MZAGA amesema kila mwanamke atambue umuhimu wa kushiriki Siku ya Wanawake Duniani mkoani TABORA inayoratibiwa na CG FM yaani CG WOMEN GALA kwa sababu watapata fursa ya kukutana na wanawake na kujadiliana mambo mbalimbali yanayowahusu kijamii na kiuchumi.

Wote kwa pamoja wametoa wito kwa wanawake wa mkoa wa TABORA kujitokeza kwa wingi kushiriki kushiriki katika sherehe hizo zitakazofanyika katika viwanja vya CHIPUKIZI mjini TABORA kwa sababu ni fursa ya kipekee kwao ya kuonana na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kujifungza mambo mengi mazuri yatakayowasaidia katika maisha yao.

Wamesema wanawake wote wa mkoa wa TABORA wanaojishughulisha na shughuli ndogondogo za kijasiriamali na wafanyakazi wa serikali wasiache kushiriki katika hafla hiyo maalumu inayowahusu wanawake.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

MARA: Mwanamke ajinyonga kwa tuhuma za wizi wa Bata
Wananchi wametakiwa kutumia fursa za elimu kukabiliana na mabadiliko ya Tabia ya nchi.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise