Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

TABORA: Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa WETCU…

  • November 7, 2017November 7, 2017

Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Mwenyekiti wa WETCU,GABRIEL MKANDALA na wenzake WATANO imetajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa wilaya ya TABORA,EMMANUEL NGWIGANA .

Kesi hiyo imetajwa jana kwa ajili ya kusikilizwa,lakini haikusikilizwa kutokana na upepelezi kutokamilika.

Wakili wa serikali,TITO MWAKALINGA ameiambia mahakama hiyo kuwa upelelezi wa shauri hilo unaendelea na kwamba jalada la kesi hiyo tayari lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka-DPP.

Mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo,GABRIEL MKANDALA baada ya kusikiliza tamko la Jamhuri kuwa bado upelelezi unaendelea ameiambia mahakama kuwa angependa kuona upelelezi unafanyika haraka na kwa haki ili wajue kama wana kesi ya kujibu au la ili waachiwe huru kwa sababu ni zaidi ya miezi saba sasa wapo rumande bila kujua hatma yao.

MKANDALA na wenzake wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi tangu Machi  mwaka huu na kesi hiyo imepangwa kutajwa tena katika mahakama ya wilaya ya TABORA tarehe 20 mwezi  huu.

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Meek Mill Ahukumiwa kwenda Jela Miaka 4.
Jamii mkoani TABORA imetakiwa kujitoa kwa hali na mali kushiriki katika kuboresha elimu.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise