Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Mkuu wa Mkoa awapongeza wazazi, walezi na walimu…

  • January 1, 2018

Mkuu wa mkoa wa TABORA,AGGREY MWANRI amewapongeza walimu,wazazi na walezi kwa kushirikiana vema kupandisha ufaulu wa wanafunzi wa darasa la saba,kidato cha nne na sita.

Katika salamu zake kwa wananchi wa mkoa wa TABORA za kumaliza mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka mpya 2018,MWANRI pia amewataka wazazi na walimu kuendelea kushirikiana kufuatilia mwenendo wa wanafunzi ili kuendelea kupandisha ufaulu kwa mwaka huu.

Akizungumzia sekta ya Afya,mkuu wa mkoa wa TABORA amesema pamoja na mapungufu yaliyojitokeza mwaka uliopita ukiwemo uhaba wa dawa na baadhi ya vituo vya afya kutowahudumia wagonjwa vizuri, serikali imejipanga kuondoa kasoro hizo.

Amesema tatizo lingine ni watu kuugua matumbo na minyoo mkoani TABORA kutokana na kutonawa mikono kabla ya kula hivyo amewataka kuzingatia hilo ili kupunguza magonjwa yanayozuilika.

Kuhusu mazingira amewashukuru wananchi wa mkoa wa TABORA,kituo cha Radio cha CGFM na waandishi wote wa habari mkoa huu kwa kushiriki vema kufanikisha kampeni ya upandaji na utunzaji wa miti mwaka 2017.

Ameongeza kuwa mwaka 2018 ili uwe wa mafanikio na maendeleo zaidi katika sekta mbalimbali,kila mmoja hana budi kusimama katika nafasi yake na kwa ushirikiano na jamii.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Wananchi mkoani TABORA watakiwa kufanya kazi kwa bidii kwa mwaka mpya 2018.
TABORA:Waumini waaswa kuwa na moyo wa shukrani kwa Mungu na Bindamu wenzao

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise