Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Waganga 86 wanaojihusisha na ramli chonganishi wakamatwa na…

  • December 26, 2017

Jeshi la polisi Mkoani TABORA limesema kuanzia januari mpaka novemba mwaka huu limefanikiwa kukamata waganga 86 ambao wanajihusisha na ramli chonganishi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa TABORA kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi WILBROAD MUTAFUNGWA amesema hatua hiyo ya misako na kuwakamata waganga kumesadia kupungua kwa mauaji

Katika hatua nyingine kamanda MUTAFUNGWA amesema, jumla ya makosa dhidi ya maadili ya jamii 602 yameripotiwa kwa mwaka huu ikilinganishwa na makosa 373 yaliyoripotiwa mwaka jana.

Aidha jeshi la polisi Mkoani hapa katika kupambana na uhalifu limefanikiwa kukamata silaha aina ya SMG MBILI na kilo 28,973 za bangi.

Hata hivyo Kamanda MUTAFUNGWA amesema sababu zinazosababisha kuwepo kwa uhalifu katika baadhi ya maeneo ni wananchi kujichukulia sheria mkononi na tamaa za kimwili kwa matukio ya ubakaji.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa TABORA kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi WILBROAD MUTAFUNGWA jeshi la polisi limejipanga kuendelea kuelimisha jamii kutojichukulia sheria mkononi

Pia kuimarisha misako na doria za magari pamoja na pikipiki kwenye barabara kuu za kuingia Mkoani TABORA.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Leo ni duru ya pili ya uchaguzi wa urais Liberia kati ya George Weah na Joseph Boakai
TABORA: Jamii yatakiwa kudumisha utaratibu wa kupenana zawadi ili kuonesha UPENDO.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise