Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Wanachi watakiwa kuacha kutumia dawa kwa mazoea

  • January 15, 2018

Wakazi wa Manispaa ya Tabora kushauriwa kwenda vituo vya huduma za afya mara wanapougua badala ya kutumia dawa kwa mazoea. Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya TABORA wameshauriwa kwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za afya wanapougua ili kupata vipimo vya kitabibu badala ya kutumia dawa kwa mazoea.

Hayo yameelezwa na mganga mkuu wa zahanati ya MORAVIAN MILUMBANI Daktari LAMECK KISULILA amesema matumizi ya dawa bila utaratibu maalum ni chanzo cha magonjwa nyemelezi mwilini na hata kusababisha vifo.

Daktari KISULILA ameitaka jamii kuwa na desturi ya kupima afya pale wanapougua kwa sababu itasaidia kubaini aina ya ugonjwa na tiba inayohitajika na pia kupunguza madhara mengine mwilini yanayotokana na usugu wa dawa.

Nao baadhi ya wananchi wa mjini TABORA wamesema wanalazimika kutumia dawa bila kupima afya zao wanapougua kutokana na hali ngumu kiuchumi.

Ameishauri jamii kuepuka matumizi ya dawa bila mpangilio maalum hasa kwa watoto kwa sababu dawa zinapozoeleka mwilini zinasababisha wawe dhaifu.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

TABORA: Wananchi watakiwa kutunza mazingira.
Kiwelu akanusha taairfa za kujiunga na Simba SC.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise