Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Wananchi walalamikia zoezi la uandikishaji wa vitambulisho vya…

  • April 16, 2018

TABORA wamelalamikia zoezi la uandikishaji wa vitambulisho vya Taifa –NIDA kwamba wanatozwa fedha nyingi tofauti na mwongozo wa serikali.

Wakazi hao wamesema kuwa zoezi la uandikishaji vitambulisho vya Taifa limekuwa na mlolongo mrefu hadi kukamilisha usajili wa kitambulisho hali inayosababisha usumbufu kwao.

Msimamizi wa zoezi la usajili na utambuzi wa vitambulisho vya Taifa mkoa wa TABORA,EMILIANA TEMU amesema watu waliyokuwa wanajihusisha na utozaji wa fedha kwenye zoezi hilo ni tamaa zao lakini kiuhalisia zoezi la uandikishaji ni bure.

Mwenyekiti wa mtaa wa KAZEHILL katika Halmashauri ya Manispaa ya TABORA,JOHN MSUMENO amesema yeye alijiandaa vizuri kwenye upande wa vifaa ili kuepusha changamoto kwa wananchi wake na kwamba changamoto zilizotokea wilayani KALIUA pengine walikuwa hawajajipanga vizuri.

Naye HAROLD KILUNGU kutoka asasi inayojihusisha na masuala ya utambuzi, utawala bora na maendeleo mkoani TABORA-TACEDE amesema zoezi la uandikishaji wa vitambulisho halijahusisha elimu ya awali kwa wananchi kama ilivyo kwa zoezi la upigaji kura ambalo hufanyika vizuri.

Msimamizi wa zoezi la usajili na utambuzi wa vitambulisho vya Taifa mkoa wa TABORA EMILIANA TEMU ameiomba kamati ya ulinzi na usalama iwajibike ipasavyo kuimarisha ulinzi katika maeneo ya kujiandikishia ili zoezi lifanyike kwa amani na utulivu.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Matumizi ya fedha za kigeni hayasababishi kushuka kwa thamani ya fedha yoyote.
Wataalamu wa silaha za sumu hawajapewa kibali kuingia Douma

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise