Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

TABORA: Wananchi watakiwa kuwasaidia na kuwajali watu wenye ulemavu.

  • February 19, 2018

Wananchi mkoani TABORA wametakiwa kuwajali na kuwasaidia watu wenye ulemavu pindi wanapokuwa katika majukumu yao ya kila siku.

Wito huo umetolewa na mkuu wa wilaya ya TABORA,Mwalimu QUEEN MLOZI,wakati akizungumza katika hafla ya kuwakabidhi vifaa mbalimbali watu wenye walemavu katika viwanja vya Taasisi ya sanamu la Mwalimu NYERERE mjini TABORA

Vifaa hivyo vimetolewa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Daktari AMONI MKOGA kwa kushirikiana na Ubalozi wa KUWAIT hapa nchini.

MLOZI pia amewasihi watu wenye ulemavu kuwa jasiri katika utendaji wa kazi zao badala ya kujishusha na kuonekana kama wametengwa na jamii jambo ambalo siyo kweli.

Mwenyekiti wa taasisi iliyotoa msaada kwa baadhi ya watu wenye ulemavu,Daktari AMONI MKOGA amesema taasisi yake imeamua kujikita kusaidia makundi maalumu baada ya kutambua makundi hayo yana uhitaji mkubwa wa msaada katika jamii.

Baadhi ya watu wenye ulemavu waliopata msaada ya baiskeli za kutembelea wamesema baskeli hizo zitawasaidia katika shughuli za mizunguko yao.

Naye mwananchi mmoja miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo mkazi wa kata ya MBUGANI,MAULIDI SHABANI ameipongeza taasisi ya Daktari,AMON MKOGA kwa kujitolea kuwasaidia makundi ya watu wenye ulemavu.

Taasisi ya Dkatari MKOGA kwa kushirikiana na ubalozi wa KUWAIT imetoa msaada wa baiskeli kwa walemavu wa miguu,fimbo za kutembelea kwa wenye uoni hafifu na cherehani za kushonea nguo kwa baadhi ya vikundi vya walemavu.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Wanafunzi wa darasa la 2-5 hawajui kusoma, kuhesabu na kuandika katika shule ya Msingi GOWEKO
Viongozi wa Serikali za vijiji, na kata watakiwa kuitisha mikutano ya kusikiliza kero za wananchi.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise