Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
International

Trump adokeza kukutana na Kim katika jumba la amani

  • May 1, 2018

Rais wa Marekani Donald Trump amedokeza kuwa mkutano wa kilele unaotarajiwa kati yake na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un ufanyike katika nyumba ya amani iliyoko katika mpaka kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini, eneo ambalo Kim alikutana na Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in wiki iliyopita.

Kupitia ukurasa wa Twitter, Trump amesema maeneo mengi katika nchi chungu nzima yanadhaniwa kuwa maeneo muafaka ya mkutano lakini anadhani nyumba ya amani itakuwa yenye ishara muhimu zaidi kuliko mkutano huo kufanyika katika nchi nyingine.

Trump anatarajiwa kukutana na Kim katika wiki chache zijazo. Hayo yanakuja huku Rais wa Korea Kusini Moon Jae in akisema Trump anastahiki kupewa tuzo ya amani ya Nobeli kutokana na juhudi zake za kuutatua mzozo juu ya mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Iran: Mpango wa sasa wa nyuklia utabaki kama ulivyo
Rais Magufuli:Serikali itaendelea kudhibiti bei za bidhaa zisipande ovyo.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise