Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Ukatili wa kingono mkoani TABORA bado ni tatizo kutokana…

  • November 16, 2017November 16, 2017

Ukatili wa kingono mkoani TABORA bado ni tatizo kwa sababu wahanga wa matukio hayo huyaficha na kuyamaliza katika ngazi ya familia bila kuyapeleka sehemu husika.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha msaada wa kisheria na haki za binadamu- PARALEGAL mkoani TABORA,MARTHA SIZYA kesi nyingi za ukatili wa kingono haziripotiwi kwenye vyombo vya sheria kwa sababu waathirika wanaona aibu kwa kutojua haki zao za msingi.

MARTHA SIZYA pia amezungumzia wajane wanaodhulumiwa mali na kufukuzwa kwenye nyumba zao na kuwataka wajane wasikae kimya kwani huo ni ukatili unaotakiwa kupigwa vita na kila mwananchi.

Naye mkazi wa Halmashauri ya Manispaa ya TABORA,JENI KAZAI amekiri kuwa vitendo vya ukatili wa kingono hasa kwa watoto vimeshamiri kwa sababu baadhi ya wazazi huwaacha watoto wao katika mazingira yasiyo salama na kwenda kwenye shughuli zao za kibiashara.

Ukatili wa kingono ni tishio la haki ya kila mtu ya kuishi kwa amani na usalama, hivyo kuna kila sababu ya kudhibiti tatizo hilo katika jamii.

Kwa mujibu wa Shirika la Haki za Binadamu la Human Rights Watch,hapa TANZANIA,kati ya watoto watatu kike,mtoto mmoja hufanyiwa vitendo vya ukatili wa kingono.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Sayari mpya inayoweza kuwa na uhai yagunduliwa.
Kansela Merkel awekwa njia panda.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise