Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Urambo, TABORA: Kijana ahukumiwa jela miaka saba kwa wizi…

  • October 19, 2017
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya URAMBO,HASSAN MOMBA amesema kuwa amelazimika kutoa adhabu hiyo ili liwe fundisho kwake na kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

Kijana BARAKA SAMSONI,mkazi  wa KIBAONI mkoani SINGIDA amehukumiwa na mahakama ya wilaya ya URAMBO kutumikia kifungo cha miaka SABA jela baada ya kukiri kuiba gari alilokuwa amekabidhiwa kuendesha.

Akisoma hukumu ya kesi hiyo,Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya URAMBO,HASSAN MOMBA amesema kuwa amelazimika kutoa adhabu hiyo ili liwe fundisho kwake na kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

Hakimu MOMBA amesema kuwa kitendo cha mshitakiwa kukiri kosa kunaonyesha ni jinsi gani hakuwa mwaminifu katika jamii inayomzunguka.

Awali upande wa mashitaka ukiongozwa na Mkaguzi wa Polisi PHILLERT PIMMA ulidai kuwa mtuhumiwa BARAKA SAMSONI alitenda kosa hilo tarehe 28 mwezi uliopita.

Ameongeza kuwa kuwa siku hiyo eneo la MAJENGO YA KATI mjini URAMBO mshitakiwa aliiba gari aina ya Toyota Land Cruser Pickup lenye namba za usajili T 659 CYK yenye thamani ya shilingi 75 milioni mali ya SUN ZHI,raia wa CHINA.

Mshitakiwa ambaye alikuwa ni dereva wa gari hilo baada ya wizi huo alikamatwa akiwa wilaya ya KAHAMA akiwa katika harakati za kutaka kuliuza kwa shilingi milioni TISA.

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Manispaa ya TABORA imesema njia mbadala itakayotumika kuweka mazingira safi ni kufuata sheria ndogo ndogo za halmashauri hiyo.
Ugonjwa wa shinikizo la jicho wazidi kushika kasi TABORA.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise