Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Ureno na Ufaransa zafuzu Kombe la Dunia Urusi 2018

  • October 11, 2017
Wachezaji wa Ureno wakifurahia baada ya kufunga goli.

Mabingwa wa Ulaya Ureno walilaza Uswizi 2-0 Jumanne mjini Lisbon na kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi kwa kumaliza kileleni Kundi B.

Iwapo wangeshindwa au kutoka sare, basi wangehitaji kucheza mechi ya muondoano kufuzu.

Lakini mabao mawili, moja la Johan Djourou aliyejifunga na Andre Silva, yalitosha kuwavusha Ureno.

Ufaransa walilaza Belarus 2-1 nakufuzu kwa kumaliza kileleni Kundi A, Swedennao wakamaliza wa pili licha ya kushindwa 2-0 na Uholanzi.

Waholanzi ambao walimaliza nafasi ya tatu Kombe la Dunia 2014 wameondolewa kwenye michuano hiyo.

Walihitaji kushinda kwa mabao saba ya wazi kuwapiku Sweden na kumaliza wa pili.

Walifunga mabao mawili pekee kuptiia Arjen Robben.

Kundi H, Ugiriki walijihakikishia nafasi michezo ya muondoano kwa ushindi wa 4-0 dhidi ya Gibraltar.

Ubelgiji ambao tayari walikuwa wamejihakikishia uongozi katika kundi hilo walilaza Cyprus 4-0 huku nyota wa Chelsea Eden Hazard akifunga mabao mawili, nduguye Thorgan akafunga moja naye mshambuliaji wa Manchester United Romelu Lukaku akafunga ukurasa wa mabao.

Mataifa ya Ulaya ambayo yamefuzu kwa sasa ni Ufaransa, Ureno, Ujerumani, Serbia, Poland, England, Uhispania, Ubelgiji na Iceland.

Kuna nafasi nne zaidi za kushindaniwa na mataifa manane kupitia muondoano wa timu nane – Sweden, Uswizi, Ireland Kaskazini, Jamhuri ya Ireland, Denmark, Italia, Ugiriki na Croatia.

Uamuzi wa nani atacheza dhidi ya nani utafanywa baada ya orodha ya viwango vya soka duniani ya Fifa kutangazwa wiki ijayo.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Ndege za kivita za Marekani zapaa rasi ya Korea
Wasiwasi kuhusu ‘wanyonyaji damu’ Malawi

Related articles

Simba Yamsajili Adam Salamba.
Roman Abrahamovich ahamia Israel.
Kipa wa Liverpool atishiwa maisha.
Haji Manara, Simba na Yanga…
Serengeti Boys wa Tanzania watwaa…
Wachezaji wanajua umuhimu wa mechi…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise