Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Vijana wametakiwa kutoogopa kwenda katika vituo na zahanati ambazo…

  • May 15, 2018May 15, 2018

Vijana wametakiwa kutoogopa kwenda katika vituo na zahanati ambazo zinatoa huduma rafiki kwao ili kupata huduma za ushauri nasaha zitakazowasaidia kuepukana na mimba za utotoni.

Hayo yamebainishwa na Muuguzi msaidizi wa zahanati ya CHEYO,BERTHA KULWA wakati akizungumzia mwitikio wa vijana kwenda katika vituo vinavyotoa ushauri nasaha na huduma ya afya ya uzazi kwa vijana akisema mwitikio wao bado ni mdogo.

Naye Muuguzi wa zahanati hiyo,GRACE SHIMBA amezitaja sababu zinazosababisha vijana kuanza ngono katika umri mdogo ambazo iwapo vijana wakipata ushauri nasaha ni rahisi kutambua jinsi gani wanaweza kuepukana na sababu hizo.

Kwa upande wao,viongozi wa madhehebu ya dini,Mchungaji wa kanisa la CVC -VICTORIUS lililopo mtaa wa KADINYA,EGON ISRAEL na Sheikh wa wilaya ya TABORA,RAMADHAN  RASHDI wamesema wanaendelea kuwahamasisha vijana na walezi kuzingatia maadili na maagizo  ya Mwenyezi Mungu na kufanyia kazi ushauri wanaopewa.

Mwaka 2016 mkoa wa TABORA ulianza kutoa huduma rafiki kwa vijana,afya ya uzazi kwa vijana,taarifa sahihi ya unasihi ya afya ya uzazi,kutambua mabadiliko yao ya kimwili,upimaji wa afya ,uchunguzi wa magonjwa ya ngono,saratani ya mlango wa uzazi na matiti,matibabu ya magonjwa ya ngono na huduma bora ya ujauzito.

Katika Halmashauri ya Manispaa ya TABORA vituo vinavyotoa huduma hizo ni CHEYO,TOWN KLINIK,KITETE na ISEVYA.

Mwandishi:- Eveline Paul.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Waumini wa dini ya Kiislamu wametakiwa kufunga siku zote za Mwezi Mtukufu wa RAMADHANI
Viongozi wa idara ya ardhi katika Halmashauri ya Manispaa ya TABORA kutakiwa kuwajibika

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise