Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Wanafunzi wa darasa la 2-5 hawajui kusoma, kuhesabu na…

  • February 19, 2018

Jumla ya wanafunzi 46 wa darasa la pili hadi la tano katika shule ya msingi GOWEKO wilayani UYUI hawajui kusoma,kuandika na kuhesabu.

Mwalimu mkuu msaidizi wa shule ya msingi GOWEKO,NAZIEL ANTHONY amesema sababu ya kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi wasiojua kusoma,kuandika na kuhesabu shuleni hapo ni utoro wa rejareja na idadi kubwa ya wanafunzi katika darasa moja.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi GOWEKO RAMADHANI JUMA amesema idadi ya wanafunzi wasiyojua kusoma, kuandika na kuhesabu ni ndogo ikilinganishwa na wanafunzi wa aina hiyo mwaka jana.

Mwalimu mkuu wa masaidizi NAZIEL ametaja mikakati ya kupuguza wanafunzi wasojua kusoma, kuhesabu na kuandika ikiwa ni pamoja na kushirikiana na wazazi kuwahimiza wanafunzi sugu kwa utoro kuhudhuria masomo.

Ameongeza kuwa mkakati mwingine alianza tangu mwezi januari ni kuwafundisha muda wa ziada kwanzia satisa alasiri hadi sakumi.

Pia idadi hiyo kubwa ya wanafunzi wasojua kusoma kuhesabu na kuandika ni miongoni mwa mambo yaliyosababisha shule hiyo kufanya vibaya katika matokeo ya darasa la saba ambapo kati ya shule 46 za wilaya ya UYUI GOWEKO ilishika nafasi ya 45.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Msafara wa Kabila wahusika kwenye ajali mbili za barabarani kwa wiki moja
TABORA: Wananchi watakiwa kuwasaidia na kuwajali watu wenye ulemavu.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise