Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Wananchi mkoani TABORA wametakiwa kutunza Misitu ili kupata mvua…

  • October 16, 2017
Msitu.

Wananchi mkoani TABORA wametakiwa kutunza Misitu ili kupata mvua za kutosha na kuuepusha Mkoa kuingia katika janga na kukosa chakula.

Wito huo umetolewa na Afisa Misitu wa Wilaya ya IGUNGA Bwana JAHULULA EDWARD akisema kuwa wananchi walio wengi hawana uelewa kwamba uharibifu wa misitu ni moja ya sababu ya kukosekana kwa mvua ambayo itasababisha kukosekana kwa chakula.

Ameongeza kuwa ni vyema wakulima wakabadilika sasa na kuanza kulima mazao ya chakula na biashara ili kujikinga na baa la njaa na kuachana na tabia ya kuchagua vyakula

Naye Bwana AMONI MOSHI amabye ni Afisa Maliasili wa Wilaya ya IGUNGA amesema kuwa kufuatia kauli ya serikali kwamba hawatatoa chakula hivyo ni vyema wananchi wakatumia njia bora za kilimo na kutunza vyakula walivyonavyo.

Nao baadhi ya wananchi katika kijiji cha MWABAKIMA Wilayani IGUNGA Bi RACHEL TUPA, JILEMBA MAGIRI na Bi ASHURA JUMA wamesema si vyema serikali kuwanyima chakula kwa sababu hali ya mvua msimu uliopita haikuwa nzuri na kusababisha uhaba wa chakula

Kila ifikapo Oktoba 16 Dunia huadhimisha siku ya chakula dunia na kauli mbiu ya mwaka huu ni kubadili mwelekeo wa wahamiaji.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Baadhi ya shule Mkoani TABORA zimeweka mazingira mazuri kwa ajili ya wanafunzi wa kike kujistiri wanapokuwa katika kipindi cha hedhi.
Makabidhiano ya miti kati ya UVISATA na uongozi wa kata ya GONGONI kama anavyotuhabarisha mwanahabari wetu.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise