Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Wananchi wa Kata ya Loya Wilaya ya Uyui Mkoani…

  • October 25, 2017
Rangi nyekundu katika Ramani inaonesha Wilaya ya Uyui.

Wananchi wa kata ya LOYA,wilaya ya UYUI mkoani TABORA wameliomba Jeshi la Polisi kupunguza masharti na vigezo ili waweze kufungua kituo cha polisi katika kata yao.

Akitoa ombi hilo kwa Kamanda wa polisi mkoa wa TABORA, Afisa Mtendaji wa kata ya LOYA, NDULILAH PANDAUYAGA amesema iwapo kituo cha polisi kitafunguliwa katika kata hiyo kitasaidia kupunguza vitendo vya uhalifu.

Diwani wa kata ya LOYA,SIZYA MASELE amesema kufunguliwa kwa kituo cha polisi katika kata yake kutasaidia kuimarisha hali ya ulinzi na usalama na kujenga woga kwa wahalifu kutoka ndani na nje ya kata hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya UYUI, SAID NTAHONDI amesema halmashauri imeunga mkono jitihada za wananchi wa LOYA na tayari imekwishatoa edha kwa ajili ya kumalizia jengo la kituo cha polisi.

Akikagua jengo la kituo hicho,Kamanda wa polisi mkoa wa TABORA Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa polisi,WILBROAD MUTAFUNGWA amesema jengo hilo lina mapungufu kidogo na iwapo yatarekebishwa basi baada ya wiki moja litafunguliwa rasmi kama kituo cha polisi.

Wananchi wa vijiji vya LOYA,MISWAKI,MMALE,MINYEZE na LUTENDE wanalazimika kutembea zaidi ya kilomita 100 kufuata huduma za kipolisi.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Zaidi ya shilingi Bilioni 23 na Milioni 200 zimetumika kunusuru kaya maskini na miradi mbalimbali ya maendeleo kutoka Mfuko wa Maendeleo ya Jamii nchini- TASAF
Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi mkoani TABORA imempongeza Rais JOHN POMBE MAGUFULI kwa kazi nzuri ya kusimamia raslimali za nchi yetu

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise