Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Wananchi wa wilaya ya NZEGA mkoani TABORA kujiandaa kwa…

  • October 5, 2017October 5, 2017
Mvua ikinyesha.

Mkuu wa wilaya ya NZEGA mkoani TABORA,GODFREY NGUPULA amewataka wananchi wa kijiji cha KISHIRI katika kata ya MWAMALA wilayani humo wanaonufaika na Mpango wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii nchini –TASAF wa kunusuru kaya maskini awamu ya tatu kuhakikisha wanajishughulisha kwa kilimo kwa kuzitumia mvua za kwanza zitakazoanza kunyesha mwishoni mwa mwezi huu.

Ametoa wito huo wakati akizungumza na wakazi wananchi juu ya kujiendeleza kiuchumi kupitia mpango wa TASAF awamu ya tatu.

NGUPULA amesema ili wanufaika hao waweze kujikwamua kiuchumi wanatakiwa kujikita katika shughuli za kilimo kwa kulima mazao yatakayoendana na hali ya hewa pamoja na kupanda mapema mwanzoni mwa  msimu wa mvua.

Amesema iwapo walengwa hao watalima mazao yao mapema itawasaidia kuvuna kwa wingi kwani yatakua yameiva kutokana na mvua zitakazokua zimenyesha mwanzoni mwa msimu wa kilimo.

Naye Kaimu Afisa wa TASAF wilayani NZEGA,ANTONY SEBASTIAN amesema zoezi la kuzinsuru kaya maskini limekua likiendelea vizuri na mabadiliko mbalimbali yameonekana kwa walengwa na kwamba wengi wao wamekua wakibuni miradi endelevu.

 

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Walimu mkoani TABORA wameiomba serikali kutatua matatizo yanayowakabili katika taaluma yao.
Mabaki ya meli ya kwanza kuzamishwa wakati wa vita vya pili vya dunia yanaonekana kupatikana katika sakafu ya Bahari ya ATLANTIKI.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise