Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Wananchi wahimizwa kushiriki kikamilifu maadhimisho ya Mei Mosi.

  • April 26, 2018

Wananchi wa mkoa wa TABORA kutakiwa kushirikia kikamilifu katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani

Wananchi wa mkoa wa TABORA wametakiwa kuonesha umoja na mshikamano kwa kushiriki kikamilifu katika maadhimisho ya ya Siku ya Wafanyakazi Duniani-MEI MOSI.

Wito huo umetolewa na Mratibu wa sherehe za Mei Mosi mwaka huu,GRATION MBEYUNGE ambaye pia ni Katibu wa chama cha wafanyakazi  wa Viwanda,Biashara,Taasisi za Fedha,Huduma na Ushauri TUICO mkoa wa TABORA wakati akizungumzia maandalizi ya sherehe hizi zitakazofanyika Kimkoa wilayani NZEGA.

Awali akizungumzia historia ya maadhimisho ya sherehe za Mei MOSI,MBEYUNGE amesema TANZANIA inaungana na nchi nyingine Duniani kuweka kumbukumbu muhimu ya wafanyakazi.

Akizungumza na CG FM,Katibu wa chama cha wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi,Teknolojia,Habari na Utafiti nchini- RAAWU na Mratibu wa Shirikisho la Vyama huru vya Wafanyakazi -TUCTA mkoa wa TABORA,ALEX BYANGWAMU amewataka wananchi wa wilaya ya NZEGA kuitumia fursa hii kikamilifu kujiimarisha kiuchumi.

Nao Baadhi ya wananchi wa wilaya ya NZEGA wamefurahishwa na hatua ya maadhimisho YA Siku ya Wafanyakazi Duniani kufanyika wilayani humo kama wanavyobainisha.

Maadhimisho ya sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani mwaka huu yanafanyika kitaifa mkoani IRINGA yakiongozwa na kauli mbiu –Kuunganishwa kwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kulenga kuboresha Mafao ya Wafanyakazi na mgeni rasmi atakuwa ni Rais Daktari JOHN POMBE MAGUFULI.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

TABORA: Jeshi la polisi lamuua Jambazi kwa risasi
Uzalishaji wa zao la Nazi washuka Zanzibar.

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise