Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise
Local

Wananchi washauriwa kwenda kwenye vituo vya msaada wa kisheria…

  • January 19, 2018January 19, 2018

Wananchi wa Halmashauri ya Manispaa ya TABORA wamehimizwa kwenda  kwenye vituo vya msaada wa kisheria na haki za binadamu ili kupata elimu itakayowasaidia kukabiliana na vitendo mbalimbali vyaunyanyasaji wa kijinsia.

Mwanasheria kutoka kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu-PARAREGAL- mkoa wa TABORA,HOSEA KAPONYA amesema kituo hicho cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu kwa mwaka 2017 kilifanikiwa kuifikisha elimu kwa jamii  kwa asilimia themanini.

Amesema mwaka jana,wakazi wa Manispaa ya TABORA mia tano na thelathini na mmoja walikwenda katika kituo hicho kwa ajili ya kupata msaada wa kisheria na walitatuliwa kero zao na kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.

GEODENS JOHN ni mmoja kati ya mwananchi aliyewahi kwenda kwenye kituo hicho na kutatuliwa changamoto iliyokuwa inamkabili amesema wasaidizi wa kisheria wana umuhimu sana katika jamii kwa sababu wanaisaidia jamii kujua haki zao za msingi.

Mwaka 2017 kituo cha msaada wa kisheria na haki za binadamu mkoani TABORA hicho kimefanikiwa kupunguza kiwango cha unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto na wanawake katika Manispaa ya TABORA kwa kutoa ushauri na elimu ya msaada wa kisheria.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa TABORA- KITETE yafungua Duka la dawa.
George Weah kuapishwa leo kuwa rais wa Liberia

Related articles

Msanii Sam wa Ukweli ameaga…
Mazishi ya pacha Maria na…
Vladmir Putin aizuru Austria.
Jeshi la Zimamoto lakanusha madai…
TABORA: Biashara ya Magimbi yashamiri…
Serikali imetenga fedha kwa ajili…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise