Skip to content
CGFM
  • Home
  • Listen Live
  • News
  • Presenters
  • Gallery
  • Advertise

Wanawake kuruhusiwa kuingia viwanja vya michezo Saudi Arabia.

  • October 30, 2017

Saudi Arabia itawaruhusu wanawake kuhudhuria michezo katika viwanga vya michezo kwa mara ya kwanza kuanzia mwaka ujao.

Familia zitaweza kuingia kwenye viwanja vitatu vya michezo vya – Riyadh, Jeddah na Dammam.

Ni hatua nyingine ya kuwapa wanawaka wa Saudi Arabia uhuru zaidi, ambao kawaida hukumbwa na ubaguzi wa kijinsia na baada ya kuendolewa marufuku ya kuendesha magari.

Mfalme Mohammed bin Salman yuko katika harakati kubwa kuifanya Saudi Arabia kuwa nchi ya kisasa na kuboresha uchumi.

Mabadiliko hayo yanaambatana na mipango mikubwa ya mabadiliko yaliyotangazwa na mfalme huyo wa umri wa miaka 32 kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi kwa taifa hilo linalotegemea mafuta, yanayojulikana kama maoni ya mwaka 2030.

Women walk on Tahlia street in the Saudi capital Riyadh on 24 September
Mwezi uliopita amri ya kifalme ilisema kuwa wanawake wanaweza kuendesha magari kwa mara ya kwanza kuanzia mwezi Juni mwaka ujao. Warsha zinafanywa na sinema zinatarajiwa kurejeshwa tena.

Siku ya Jumatano Prince Mohammed alisema kurejeshwa kwa uislamu wa wastani ni kiungo muhimu cha kuifanya nchi kuwa ya kisasa.

Alisema kuwa asilimia 70 ya watu nchini Saudi Arabia wana umri wa chini ya miaka 30 na alisema kuwa wanahitaji maisha ambayo yanastahili dini.

Lakini wadadisi wanasema mipango haitakosa pingamiza.

Wanawake nchini Saudi Arabia bado ni lazima wafuate mitindo ya mavazi na wasikuwe na mahusiano na wanaume wasiostahili.

Share this:

  • Click to share on Twitter (Opens in new window)
  • Click to share on Facebook (Opens in new window)
  • Click to share on Google+ (Opens in new window)

Related

Serikali mkoani TABORA imewaonya wanaokatisha msomo ya wanafunzi kwa kuwapa mimba au kuwatumikisha.
Mamia ya wafuasi wa IS wakamatwa Uturuki.

Related articles

Mabaki ya ndege iliotoweka na…
Refa Mkenya aliyeteuliwa na Fifa…
Rais Madagascar ateuwa waziri mkuu…
Bodi ya usimamizi wa shule…
Mchungaji auawa akiwabatiza waumini Ziwani
Volkano yasabisha vifo vya watu…

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

On Air Now

Download CG Google App here

CLICK TO PLAY CG ONLINE TV

Advertise here

ABOUT US

CG FM RADIO is the radio station that based in Tabora – Tanzania that targets all age groups. Due to its moral observation and ethical programs, CG FM radio continues to have a lot of audience which makes us the best on western zone.

YOU ARE HOME

TWITTER

My Tweets

Menu

  • HOME
  • News
  • Listen Live
  • Advertise